Thursday, September 20, 2012

MAPENZI NA MAGARI


Sijui ni wazimu au nikupagawa ?.
Lakini Edward Smith Washington Marekani anasema yeye ni Mzima na akili zake.
Edward Smith hana haja na mpenzi anayetembea kwa miguu miwili.
Mmarekani huyo anasema sio hata hana hisia , anazo tena nyingi. Lakini sio kwa binadamu.
Edward Smith ambaye ni mtunzi wa mashairi ana fanya mapenzi na gari, kufanya mapenzi kwa maana halisi ya kufanya mapenzi . Smith anasema akiwa na hamu hufanya na gari kama vile nissan, pudjo, mercidez benz na vitu kama hivyo, lakini sio mtu.
Shirika la habari la Reuters limeripoti kwamba kwa wakati huu Edward Smith anafanya mapenzi na gari lake jeupe la Volkswagen Beetle .
Usiniulize anafanya mapenzi vipi na magari. Mimi sijui.
Lakini Edward Smith amefichua kuwa mara ya kwanza kufanya mapenzi na gari alikuwa na umri wa miaka 15, tena gari la babake aina ya Range Rover.
Na kwa yale mahaba aliyonayo kwa mpenzi wake wa sasa Volkswagen Beetle ambaye ameeishi naye kwa miaka mitano,amelibandika kipenzi chake jina la Vanilla.
My sweet vannila wala sio my sweet Elizabeth.
My sweet Elizabeth kanda bongoman.
chanzo:bbc

1 comment: